TANGAZA NASISI

Breaking News

Kiwanda cha Mount Meru Millers Yapigwa faini sakata la Uchafuzi wa Mazingira , Kinabo atia Neno

Diwani wa Kata  ya Themi Mh. Melance Kinabo akiambatana na Wajumbe wa Serikali za Mtaa wa Kambarage , Bwana afya Kata  ya Themi na uingozi wa mtaa wakitatua tatizo la utiririshwaji holela wa Maji machafu kutoka kiwanda  cha SUNOLA kwenda kwenye Makazi ya wananchi.
 Wananchi katika mtaa wa Kambarage kwenye kata  ya Themi Jiji la Arusha wamelalamikia kitendo cha kiwanda cha SUNOLA kutiririsha Maji machafu nakupelekea harufu mbaya uharibifu wa mazingira na miundo mbinu ya barabara.

Wakizungumza na Idea Radio wananchi hao wamesema suala hilo  limekuwa sugu kwenye eneo hilo na kwamba wanapata adha ya kukumbana na harufu Kali ambayo hutokana na muozo wa Maji hayo machafu ambayo yanadaiwa kufunguliwa nyakati za usiku .

Eneo la barabara  ambayo Maji hayo machafu yanatiririkia...

Aidha Diwani wa Kata  ya Themi Jiji la Arusha Mh. Melance Kinabo amesema wameipa Kiwanda hicho Onyo  kwa kuziba matundu yote inayopitisha maji  hayo kuelekea barabarani na kuhakisha Maji yote machafu kutoka kiwandani hapo hayatoki nje badala Yake watafute mbadala.
Zoezi la Uchimbaji wa mitaro maalum ya Kutiririsha Maji kwenda kwenye chemba zikiwa zinaandaliwa...

Diwani Kinabo amesema "Tunahitaji viwanda lakini pia afya na maisha ya wananchi wetu ndo jambo la kwanza hivyo tumieiomba Kiwanda hichi  kutekeleza maazimio hayo.." Alisema Mh. Kinabo


Naye katika Taarifa Yake Afisa Afya Kata  ya Themi Akaeleza Historia  ya tatizo tangu  lilipoanza kulalamikiwa ambapo  Taarifa hiyo imedai kuwa Kiwanda hicho kilishapigwa faini ya shilingi za Tanzania laki mbili (200,000) kama adhabu Fedha ambazo wameshalipia.

Jitihada zetu za kuwapata uongozi wa Kiwanda hicho ziligonga mwamba ili kuzungumzia tuhuma hizo huku jitihada zaidi zikiwa zinaendelea.

No comments